Jumatano, 1 Juni 2016

Madereva bodaboda wananyofowa 'side mirror'



PIKIPIKI nyingi  zinazotoa huduma za usafiri wa abiria katika mji wa Morogoro zimenyofolewa vioo ya upande 'Side Millor’ zinazowezesha dereva kuona kitu kinachokuja nyuma yake akiwa barabarani hali inayohatarisha maisha ya dereva na abiria wa bodaboda.

Mwandishi wa habari hizi  alishuhudia bodaboda nyingi ambaz ziko katika  vituo mbalimbali vya bodaboda , umebaini kuwa kati ya pikipiki 10 zinazoengeshwa , saba hazina  upande kioo,  hali imezifanya  kuwepo kwa  idadi kubwa ya pikipiki zenye mapungufu hayo.

Mmoja wa madereva wa bodaboda, wa mtaa wa Mafisa Jumanne Mayala alisema yeye  ameondoa upande kioo  kwenye pikipiki yake ili kutokana na adha aliyokuwa anaipata anapotaka kupita maeneo yenye barabara nyembamba na kupenya  kati kati ya magari.

“ Upande Kioo ama tunavyoita vioo vya pembeni , zinazuia uwezo wa
kupenya mwenye msongamano wa magari  kutokana na upana wake “ alisema
Mayala.

Mbali na huyo, Dereva mwingine wa  bodaboda  wa mtaa wa  Uguu , Kata
ya Uwanja wa Taifa aliyejitambulisha kwa jina la Hassan Juma , alisema
yenye aliondoa ili  kupata urahisi wa kuingiza pikipiki ndani ya chumba la kulaza kutokana na baadhi ya milango upana wake kuwa mdogo.

Juma alisema madereva wengi wa  pikipiki za biashara maengesho yao ni
kwenye makazi wanakoishi.

Naye Dereva wa bodaboda mkazi wa Mwembesongo aliyejitambulisha kwa
jina la Charles  Frank , alisema  upande kioo  katika pikipiki  vina
umuhimu wake  katika kusaidia usalama wa dereva na abiria .

Hivyo alisema kuondoa  Upande Kioo  mwa pikipiki ni  makosa ya sheria
ya usalama barabarani na  pia ni jambo hatarishi  kwa mwendeshaji
kutokuwa salama akiwa barabarani.

“ Mara nyingi  upande kioo  vinasaidika kuona nyuma kitugani kinakuja
na kipo umbali gani na pia kusadia wakati wa kutaka kuingia  upande
mwingine wa barabara  bila kugeuka nyuma “ alisema Frank .

Kwa upande wake, Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani mkoa wa
Morogoro, Boniface Mbao , alisema kuwa, kuondoa  upande kioo ‘ Side
Millor ‘ katika  pikipiki ni kosa kisheria na kwamba  opereshani
maalumu inaendelea kufanyika kuhusiana  makosa hayo .

Mbao alisema ,  pikipiki za aina hiyo  zinapokamatwa zinahesabika
zinaendeshwa barabarani zikiwa na ubovu  na wakosaji wa makosa hayo
watatozwa adhabu kwa mujibu wa sheria za makosa ya usalama barabarani.

Kutokana na pikipiki kutozingatia sheria za usalama barabarani, mwezi Mei katika operesheni iliyofanywa na polisi wamekamata waendesha pikipiki 1,189 kwa kutoava kofia ngumu, 248 wanaendesha bila bima, 168 hawana leseni na makosa mngine 955.

Mwisho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni