USALAMA KWANZA-BLOG
Jumatano, 31 Agosti 2016
Sheria dhaifu zinawapa kiburi madereva wa bodaboda
Na Shadrack Sagati
Afisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoa wa Iringa, Patel
Ngereza
amesema sheria
zinazotumika mahakamani kuwahukumu
wakosaji wa makosa ya barabarani ni dhaifu.
Akizungumza na gazeti hili, Ngereza alisema madereva
wengi wamezoea kulipa faini na wanaona kama ni jambo la kawaida.
“Ipo haja kwa mahakama kuwatoza faini na kuwafunga
kwa makosa yanayofikishwa mahakamani, hii itawaogopesha na kuwafanya wazingatie
sheria,” anasema.
Kuhusu sheria hizo, Kamanda wa Kikosi cha Usalama
Barabarani anasema mapendekezo yao faini ianzie Sh 100,000 na kifungo kiwe cha
zaidi ya mwaka mmoja.
“Kati ya Machi na April mwaka huu makamanda wa
usalama barabarani tulikutana Morogoro na tukaja na mapendekezo hayo mapya ya
adhabu za makosa ya barabarani, tunaomba wabunge watusaidie kuyapitisha pale
yatakapofikishwa bungeni” anasema.
Anasema takwimu za kimataifa zinaonesha asilimia 51
ya ajali zote duniani zinasababishwa na pikipiki kwahiyo kama nchi inataka iwe
huru na ajali ni lazima sheria za adhabu za makosa ya barabarani ziwe
zinafanyiwa mabadiliko ya mara kwa mara.
Mwenyekiti wa Chama cha Bodaboda (CBBI) mkoani Iringa
Hassan Abdul akizungumzia adhabu za hizo, alisema ukubwa wa adhabu hizo unashawishi rushwa na
zinawafanya baadhi ya madereva wasibadilike.
“Rushwa imewafanya baadhi ya madereva hao wawe
watukutu, waendelee kutozingatia sheria za usalama barabarani. Pamoja na
kutozingatia sheria hizo utukutu wa madereva hao umevuka mipaka hadi kwa abiria
wao,” anasema.
Naye Mwenyekiti wa UBBM Makarius Changula ambaye
anakiri kuwahi kukamatwa kwa kuendesha pikipiki isiyo na bima anasema adhabu
kwa madereva wa bodaboda ziangaliwe upya kwani ni kubwa.
“Adhabu ni kubwa sana, zinachochea rushwa na nikiri
baadhi ya askari wa pikipiki, wanapokea sana rushwa kwasababu wanajua hatuwezi
kulipa faini kubwa wanazotutoza, hiyo maana yake ni kwamba tutaendelea kufanya
makosa ya barabarani na kwa kuzingatia madereva wapya wa bodaboda wanazaliwa
kila siku na kuingia barabarani bila kujali sheria zilizopo,” alisema.
Anasema mfumo wa utekelezaji wa sheria za usalama
barabarani na zile za Sumatra ni wa kikandamizi kwasababu umeshindwa
kuzitofautisha bodaboda ambacho ni chombo cha chini kabisa cha moto na vingine
vikubwa zaidi yake.
Changulla anapendekeza faini kwa kosa la barabarani
au lolote linalohusiana na biashara yao iwe Sh 10,000 kwa kosa moja.
Akizungumzia pikipiki zinazokamatwa kwa makosa
yanayohusiana na ukosefu wa stika za Bima, Changulla anasema gharama yake ni Sh
65,000 kwa mwaka, lakini pamoja na wamiliki wengi wa bodaboda hizo kulipa kiasi
hicho kila mwaka, hakuna rekodi inayoonesha kuna msaada wanaopata kutoka katika
makampuni ya Bima pindi wanapopata ajali.
“Pikipiki yako iharibike, dereva au abiria wako
uvunjike au kupata madhara mengine yoyote yale, hakuna fidia yoyote. Sasa
kwanini tuendelee kulipia stika za Bima, malipo hayo ni kwa ajili ya
kumnufaisha nani kama hawana msaada wowote,” anasema.
Anasema katika ofisi ya chama chake, kuna madereva
wanachama wa UBBM zaidi ya 120 waliopata ajali katika mazingira tofauti lakini
hakuna hata mmoja aliyepata fidia toka katika hayo makampuni ya Bima.
ends
Jumanne, 5 Julai 2016
Jumatano, 1 Juni 2016
Madereva bodaboda wananyofowa 'side mirror'
PIKIPIKI nyingi zinazotoa huduma za usafiri wa abiria katika
mji wa Morogoro zimenyofolewa vioo ya upande 'Side Millor’ zinazowezesha dereva
kuona kitu kinachokuja nyuma yake akiwa barabarani hali inayohatarisha maisha ya dereva na abiria wa bodaboda.
Mwandishi wa habari hizi alishuhudia bodaboda nyingi ambaz ziko katika vituo mbalimbali vya bodaboda , umebaini kuwa kati ya pikipiki 10 zinazoengeshwa , saba hazina upande kioo, hali imezifanya kuwepo kwa idadi kubwa ya pikipiki zenye mapungufu hayo.
Mmoja wa madereva wa bodaboda, wa mtaa wa Mafisa Jumanne Mayala alisema yeye ameondoa upande kioo kwenye pikipiki yake ili kutokana na adha aliyokuwa anaipata anapotaka kupita maeneo yenye barabara nyembamba na kupenya kati kati ya magari.
“ Upande Kioo ama tunavyoita vioo vya pembeni , zinazuia uwezo wa
kupenya mwenye msongamano wa magari kutokana na upana wake “ alisema
Mayala.
Mbali na huyo, Dereva mwingine wa bodaboda wa mtaa wa Uguu , Kata
ya Uwanja wa Taifa aliyejitambulisha kwa jina la Hassan Juma , alisema
yenye aliondoa ili kupata urahisi wa kuingiza pikipiki ndani ya chumba la kulaza kutokana na baadhi ya milango upana wake kuwa mdogo.
Juma alisema madereva wengi wa pikipiki za biashara maengesho yao ni
kwenye makazi wanakoishi.
Naye Dereva wa bodaboda mkazi wa Mwembesongo aliyejitambulisha kwa
jina la Charles Frank , alisema upande kioo katika pikipiki vina
umuhimu wake katika kusaidia usalama wa dereva na abiria .
Hivyo alisema kuondoa Upande Kioo mwa pikipiki ni makosa ya sheria
ya usalama barabarani na pia ni jambo hatarishi kwa mwendeshaji
kutokuwa salama akiwa barabarani.
“ Mara nyingi upande kioo vinasaidika kuona nyuma kitugani kinakuja
na kipo umbali gani na pia kusadia wakati wa kutaka kuingia upande
mwingine wa barabara bila kugeuka nyuma “ alisema Frank .
Kwa upande wake, Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani mkoa wa
Morogoro, Boniface Mbao , alisema kuwa, kuondoa upande kioo ‘ Side
Millor ‘ katika pikipiki ni kosa kisheria na kwamba opereshani
maalumu inaendelea kufanyika kuhusiana makosa hayo .
Mbao alisema , pikipiki za aina hiyo zinapokamatwa zinahesabika
zinaendeshwa barabarani zikiwa na ubovu na wakosaji wa makosa hayo
watatozwa adhabu kwa mujibu wa sheria za makosa ya usalama barabarani.
Mwandishi wa habari hizi alishuhudia bodaboda nyingi ambaz ziko katika vituo mbalimbali vya bodaboda , umebaini kuwa kati ya pikipiki 10 zinazoengeshwa , saba hazina upande kioo, hali imezifanya kuwepo kwa idadi kubwa ya pikipiki zenye mapungufu hayo.
Mmoja wa madereva wa bodaboda, wa mtaa wa Mafisa Jumanne Mayala alisema yeye ameondoa upande kioo kwenye pikipiki yake ili kutokana na adha aliyokuwa anaipata anapotaka kupita maeneo yenye barabara nyembamba na kupenya kati kati ya magari.
“ Upande Kioo ama tunavyoita vioo vya pembeni , zinazuia uwezo wa
kupenya mwenye msongamano wa magari kutokana na upana wake “ alisema
Mayala.
Mbali na huyo, Dereva mwingine wa bodaboda wa mtaa wa Uguu , Kata
ya Uwanja wa Taifa aliyejitambulisha kwa jina la Hassan Juma , alisema
yenye aliondoa ili kupata urahisi wa kuingiza pikipiki ndani ya chumba la kulaza kutokana na baadhi ya milango upana wake kuwa mdogo.
Juma alisema madereva wengi wa pikipiki za biashara maengesho yao ni
kwenye makazi wanakoishi.
Naye Dereva wa bodaboda mkazi wa Mwembesongo aliyejitambulisha kwa
jina la Charles Frank , alisema upande kioo katika pikipiki vina
umuhimu wake katika kusaidia usalama wa dereva na abiria .
Hivyo alisema kuondoa Upande Kioo mwa pikipiki ni makosa ya sheria
ya usalama barabarani na pia ni jambo hatarishi kwa mwendeshaji
kutokuwa salama akiwa barabarani.
“ Mara nyingi upande kioo vinasaidika kuona nyuma kitugani kinakuja
na kipo umbali gani na pia kusadia wakati wa kutaka kuingia upande
mwingine wa barabara bila kugeuka nyuma “ alisema Frank .
Kwa upande wake, Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani mkoa wa
Morogoro, Boniface Mbao , alisema kuwa, kuondoa upande kioo ‘ Side
Millor ‘ katika pikipiki ni kosa kisheria na kwamba opereshani
maalumu inaendelea kufanyika kuhusiana makosa hayo .
Mbao alisema , pikipiki za aina hiyo zinapokamatwa zinahesabika
zinaendeshwa barabarani zikiwa na ubovu na wakosaji wa makosa hayo
watatozwa adhabu kwa mujibu wa sheria za makosa ya usalama barabarani.
Kutokana na pikipiki kutozingatia
sheria za usalama barabarani, mwezi Mei katika operesheni iliyofanywa na polisi
wamekamata waendesha pikipiki 1,189 kwa kutoava kofia ngumu, 248 wanaendesha
bila bima, 168 hawana leseni na makosa mngine 955.
Mwisho.
Polisi yavuna mamilioni kwa makosa ya barabarani
POLISI mkoani Morogoro kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani imeendesha operesheni maalumu ya kukamataji wa makosa ya usalama barabarani na kufanikiwa kukamata idadi kubwa ya makosa 9,612 ya magari na pikipiki katika kipindi cha mwezi Mei, mwaka huu.
Kutokana na idadi hiyo ya makosa ya usalama barabarani, jumla ya Sh milioni 288.3 zimepatikana kutokana na tozo mbalimbali kwa makosa ya magari na pikipiki mkoani Morogoro.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei alisema hayo hivi karibuni mjini hapa, kuwa katika oparesheni maalumu ya ukamataji wa makosa ya usalama barabarani ilifanyika kuanzia Mei Mosi hadi mwishoni mwa mwezi huo.
“Polisi mkoa wa Morogoro kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani kimeendesha oparesheni maalaumu kwa mwezi Mei na kuweza kukamata jumla ya makosa 9,612 ya magari na pikipiki kisha kukusanya jumla ya Sh 288,360,000 kutokana na tozo mbalimbali” alisema Kamanda Matei.
Kamanda Matei alitaja aina ya makosa ya magari ya mwendokasi ni 2,661, ubovu wa magari 988, kukiuka ratiba 275 , kuzidisha abiria makosa 113, magari kutokuwa na bima 114 na makosa mengineyo ni 2,908.
Hivi karibuni , Kamanda huyo alisema katika makosa ya usalama barabarani katika oparesheni maalumu ya ukamataji wa makosa hayo iliyofanyika Aprili mosi hadi 30, mwaka huu , jumla ya makosa 7,838 kwa magari na pikipiki yakikamatwa.
Kutokana na makosa hayo zilikusanywa jumla ya fedha taslimu Sh 235,140,000 kutokana na tozo mbalimbali , ambapo makosa ya magari yalikuwa ni mwendo kasi 1,801, ubovu wa magari 909, kukiuka ratiba ya safari 230, kuzidisha abiria 117, kutokuwa na bima 111 na makosa
mengineyo ni 2,110.
ends
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)